· Sehemu ya kitalu iwe wazi, mbali na kivuli na kiwe karibu na chanzo cha maji.
· Tengeneza tuta la kubwa wa 1m x 2m . Urefu na idadi ya matuta hutegemea kiasi cha
mbegu. Kiasi cha mbegu kwa hectare moja ni kilo 6 au 2 kg kwa eka.
· Weka samadi iliyooza vizuri kiasi cha debe moja au mchanganyiko wa mbolea ya TSP na
CAN (200gm) kwa uwiano wa 1:1 kwenye tuta changanya vizuri na udongo.
· Sia mbegu kwenye mistari kwa nafasi ya 1 sm x 20 sm. Tawanya mbegu vizuri wakati
wa kusia ili miche isisongamane.
· Funika mbegu na weka matandazo ya nyasi kavu juu ya tuta na mwagiliwa maji. Udongo
unatakiwa kuwa na unyevu kiasi mpaka mbegu ziote.
· Nyasi ziondolewe mara tu mbegu zikiota (siku7-10 kutegemea hali ya hewa).
· Miche itunzwe vizuri na kitalu kiwe katika hali ya usafi.
· Miche imwagiliwe maji mpaka ifikie umri wa kupandikiza shambani (wiki 5-6)
![Image result for kitalu cha kitunguu](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiT7ceD268mRjI8oKE51QfJnpgbnnj8JKub8T8OtekPMoQvrb4RPmIxHkMrHa0U_1u3pBoEeast678SVTlY14WfSl7idfsuYc_QVWjVWCcUybQ6pCgxGK5uBrjmdcKZ8I9xboFTlAR1HqBX/s1600/r1.jpg)
0 comments:
Post a Comment